madaktari kenya wakataa nyongeza ya mishahara ya serikali
Mgomo huo umelemaza huduma katika hospitali na zahanati za umma.
Rais Uhuru Kenyatta alikutana na wawakilishi wa chama cha taifa cha madaktari hao Jumanne na kupendekeza nyongeza ya mshahara na marupurupu ya madaktarii kwa angalau $560 (£450).
Hilo lingesababisha madaktari wanaoanza kazi kulipwa takriban $2,000 kila mwezi.
Viongozi wa chama hicho, ambao walikuwa wameahidi kutangaza msimamo leo, walisema pendekezo la serikali linawafaa madaktari lakini kuna baadhi ya mambo ya kuwafaa wananchi ambayo yameachwa nje.
Madaktari wanaitaka serikali kutekeleza makubaliano ya mishahara na marupurupu yaliyotiwa saini mwaka 2013.
BBCswahili
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni